Habari
yako rafiki na heri ya mwaka mpya mwaka 2017.
Napenda
kukukaribisha sana katika blog hii ambayo kusudi lake ni kukupa hamasa juu ya
mafanikio katika maisha tulionayo hapa katika ulimwengu huu.
Changamoto zimekuwa nyingi kwenye maisha hata kusababisha watu wengi kutofikia malengo
ambayo wamejiwekea kwa mda mwingi.Tumaini lipo rafiki kuwa waweza fikia malengo
yako kiurahisi hata kama changamoto ni nyingi kiasi gani kama
tu utaruhusu mawazo chanya kufanya kazi katika ubongo wako na kuona mbali kama
tai na kugundua kuwa mbele ya changamoto ulizo nazo ndipo mafanikio yako
yallipo.
Huwa
kwenye maisha kila kinachomtokea mtu humtokea kwa sababu na mtu asipofikiria
kwa makini kuwa changamoto anayokumbana nayo imetokea kwa sababu huweza
kujikuta anakuwa
mnyonge, mtu mwenye huzuni na kulia kila wakati anapofikiria changamoto alizo
nazo pia anaweza kujiona kuwa ni mtu
asie faa katika jamii pia mwingine hufikia hatua ya kutokujiamini kuwa ana uwezo wa
kufanya kitu flani na kufanikiwa vizuri zaidi kwasababu tu kila
alipokuwa akijaribu kufanya kitu flani na kushindwa kufanikiwa mara kadhaa akaamua kukata tama na kujiona kuwa hawezi
tena kufanya kitu na akafanikiwa katika maisha na hii ni hatua ambayo si nzuri
katika maisha ya mafanikio.
Hivi
wajua kuwa hakuna mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri kwa namna ya hali ya
juu, kubadili maisha ulio nayo na kuweka malengo makubwa naya hali ya juu na
kuyafikia kama wewe,je
wajua hilo? Waweza kusema hapana kwa
haraka punde tu uliposoma hapo juu kuwa una uwezo mkubwa,je wajua kwanini
umesema huna uwezo huo punde uliposoma hapo juu?
Nikwasababu ya kuto kujiamini, kuto kujaribu,kuto kujikubali jinsi ulivyo,
lakini napenda nikwambie kuwa unao uwezo hujafaham tu kuwa unao uwezo. Kwenye
maisha mawazo hasi yanayoonyesha nia ya kushindwa ni hatari sana kwenye mafanikio wapaswa
usikubaliane nayo hata kidogo ondoa dhana ya kushindwa weka nia ya kuwa unaweza
jaribu mara nyingi kufanya kitu
hata ukishindwa mara kadhaa jaribu kwani kuna msemo unaosema ”practice makes parfect” kadri unavyofanya kitu unajijengea uwezo wa kukiweza.
Jua
katika maisha hakuna alieubwa akawa anajua moja kwa moja kuweka malengo na kuyafikia bali watu
wanajifunza kutokana na kukosea kwao na pia wanajifunza kutoka kwa wengine namna
wanavyofanya vizuri na kufanikiwa.chamsingi jikubali jinsi ulivyo, usikubali
kukatishwa tama na mtu yeyote,jifunze kutoka kwa wengine, toa mawazo ya
kushindwa kwenye akili yako kwakuwa wewe si wakushindwa.
Mpendwa mwisho kabisa jua kuwa wewe
ni wapekee kuliko mtu awae yote na pia una uwezo mkubwa kuliko mtu awae yote na unaweza kuwa mfano mzuri na mtu wa
kuigwa katika jamii kwa mafanikio ambayo utayapata kutokana na juhudi zako
ambazo ni tofauti na za mtu yoyote. Nakutakia mafanikio mema.
Mpendwa
naomba umshirikishe mtu mwingine ujumbe huu ili uwe hamasa na msaada katika maisha
yake.
Emmanuel Daud
Simu:
0679329339
Email:
daude950@gmail.com
Post a Comment