MAMBO MAWILI (2) HATARI KATIKA MAISHA YA MAFANIKIO

Habari rafiki karibu tena katika makala ya leo ambayo ni yakuvutia na ya pekee katika maisha yako karibu sana.

Rafiki katika maisha waweza kukubaliana na mimi kuwa kuna vitu hatari ambavyo jamii au hata wazazi wetu hutukataza kuwa tusivifanye kwakuwa ni hatari katika maisha mfano wizi ni kitu ambacho wazazi, walezi na jamii kwa ujumla hutuambia kuwa ni hatari katika maisha.

Lakini pia katika engo au eneo la mafanikio katika maisha pia kuna vitu ambavyo ni hatari na watu wengi wamekuwa wakivikumbatia pasipo kujua kuwa ndo chanzo cha maisha yao kutokuwa vizuri na kuto kuwa na uwezo wa kuona mbali kimalengo na kimawazo maishani mwao, hebu rafiki karibu usome vitu hivyo ambavyo ni hatari na yawezekana na wewe ndivyo ulivyo vikumbatia mpaka sasa pasipo kujua kuwa ndio chanzo cha maisha yako kuwa hivyo yalivyo sasa.

Mambo hayo hatari ni haya yafuatayo;

1. kukubaliana na maisha ulionayo bila kutafuta suluhisho la kujitoa kwenye maisha hayo ulionayo.

Rafiki yawezekana ulemavu ulionao ndio unaokufanya ukubaliane na maisha ulionayo maisha ambayo si maisha mazuri maisha  yenye  kudharauliwa  maisha yenye kunyanyaswa na kutengwa na jamii au yawezekana ni umaskini ulionao katika familia yenu ndio unaokufanya ukate tama kiasi hiko na kuamua kuridhia maisha ulio nayo na kuishi bila kufikiria kuwa nini ufanye ili kujikomboa kutoka katika maisha hayo au yawezekana una elim ambayo unahisi ni ndogo ambayo si kama ya mtu flani hivi unaeishi nae jirani ambae yawezekana yeye ana DIPLOMA, PHD, MASTERS na nk, au yawezekana ni kwasababu wewe ni mtoto yatima huna wazazi ambao ulikuwa unawategemea sana kwa kila jambo katika maisha yako  ni kweli inauma kuwakosa wazazi katika maisha yawezekana ndomana unaamua kukubaliana na hali mbaya ya umaskini ulionayo, au yawezekana ni ugonjwa ulionao ambao yawezekana umeambiwa na madaktari kuwa huwezi kupona tena, ndomana umeamua kukata tama na kuamua bora liende kwa maisha ulionayo ulio nayo, yawezekana ni mambo mbalimbali ambayo unayafikiria akilini mwako  mda huu unaposoma makala hii.

Rafiki nikweli mambo hayo unayokumbana nayo yanauma sana nikweli yanauma, lakini rafiki katika maisha kuna changamoto nyingi kama hizo ulizo nazo lakini  napenda nikwambie kuwa changamoto na shida ulizonazo wapaswa uzishinde sikuzote usikubali zikushinde hio ndio kanunini ya mashujaa
waliofanikiwa, unapaswa utumie changamoto ulizo nazo kama FURSA na njia ya kukufanya ufikie mafanikio makubwa na yenye kukupatiya furaha, ulemavu, umaskini, kuwa na elim ndogo, au kutokuwa na elim kabisa, uyatima, ugonjwa na vingine vingi vinavyokukumba usikubali kamwe vikufanye ukubaliane na maisha mabaya ulionayo sasa bali kwa hivyo hivyo ulivyo unaweza kuupindua ulimwengu juu chini kwa mawazo, akili na ujuzi mkubwa Mungu aliouweka ndani ya ubongo wako na kufanya maisha mabaya ulionayo yawe maisha mazuri ya kutamaniwa na kila mtu maishani.

Rafiki sasa ni muda wa kutumia hali ulio nayo, shida ulizo nazo, changamoto ulizo nazo kama fursa si kama changamoto tena katika maisha yako ili kupata mafanikio, kamwe usikubali kukubaliana na maisha hayo ulio nayo na kuamua kubweteka bila kutafuta suluhu au njia ya kupata maisha bora.

2. kuto kujiamini na kujikubali jinsi ulivyo.

Maisha yenye mafanikio yana uhusiano mkubwa na jinsi unavyo jiamini na kujikubali, watu wengi
wamekuwa wanashindwa kufanikiwa au kufikia malengo yao si kwasababu hawana uwezo huo
wanao lakini ni kwasababu tu hawajiamini wala kujikubali.

Kuto kujiamini huweza kukufanya usiwe na uwezo mkubwa wa kufikiri mbali, pia hukufanya kila unalolifanya ujione kuwa unakosea na kibaya zaidi hali ya hofu hujengeka ndani ya ubongo wako na kupelekea kila unachotaka kukifanya punde tu unapokifikiria kwenye ubongo wako unajikuta unajikosoa mwenyewe kuwa huwezi kufanya kitu unachokiwaza kukifanya si kweli kuwa hukiwezi unakiweza ila ulishajijengea kuto kujiamini.
Pia hali ya kuto kujikubali jinsi ulivyo ni hatari kwako hupoteza uwezo wa wewe kufanya lolote mbele ya watu, watu wengi wanajidharau na kujitenga katika jamii kisa ni walemavu, au kisa wao ni maskini, au kisa wao ni kabila flani ambalo wanahisi ni kabila linalodharauliwa sana na watu.

Rafiki muda wa kujidharau na kuto kujikubali ulivyo sio huu huu nimuda wa kujiamini na kujikubali ulivyo watu waliowengi ambao nimatajiri duniani ukiangalia historia zao ni watu waliokuwa na ulemavu kama ulionao, walikuwa maskini kama wewe, walikuwa wanadharauliwa kama wewe na vingine vingi ambavyo sijavitaja lakini siri kubwa ya kufanikiwa kwao ni kuwa ingawa walikuwa na kasoro zote hizo hawakujidharau walijiamini na kujikubali jinsi walivyo ndiomana hii leo tunawasoma na kuwafaham kuwa ni watu mashuhuri duniani hata wewe unaweza kuwa kama wao chukua hatua leo jiamini, jikubali ulivyo utafanikiwa usiwaze kuwa jamii inakusemaje bali waza kuwa ufanye nini ili jamii ikutolee mfano kwa kila waliongealo kutokana na mafanikio ulio nayo na jinsi unavyojikubali na kujiamini ingawa una kasoro.

Juwa kuwa shida, umaskini au kasoro uliyonayo ni FURSA kamwe usiiangalie wala kuitumia kama shida au kasoro iangalie kama fursa maishani mwako.

Nashukuru rafiki kwa kusoma makala hii natumaini imebadilisha maisha yako na kuleta mafanikio makubwa yenye furaha maishani mwako.

Naomba pia umshirikishe mwenzako ujumbe huu ili uweze kumsaidia katika maisha yake ya mafanikio.

Nakutakia mafanikio mema rafiki.

Emmanuel Daud
Waweza kutoa maoni au ushauri kupitia;
Sim: 0679329339 | 0743782086
Email: daude950@gmail.com




No comments