JITAHIDI KUYAISHI MALENGO YAKO USIYASHI MALENGO YA WENZAKO.
Habari rafiki naamini umzima wa afya, karibu katika makala ya
leo tena katika Blog hii ya ONA – MBALI.
Leo napenda tujifunze jambo kubwa linalowafanya wengi
washindwe kufikia njozi na malengo yao, jambo lenyewe si jingine ni “KUYAISHI
MALENGO YA WENGINE BADALA YA KUYAISHI MALENGO YAKO”
Rafiki katika maisha watu wengi huweka malengo tena makubwa
na yenye kuvutia kiasi kwamba mtu akikuhadisia waweza kujihisi kuwa wewe huna
malengo makubwa kama alionayo mtu huyo, lakini chakushangaza kadri siku
zinavyokwenda ukimfwatilia mtu huyo ili kujua kuwa amefikia wapi katika yale
malengo aliyokuhadisia waweza kumkuta yuko vile vile na hata chakushangaza zaidi
waweza kumkuta mtu huyo anazidi kuwa na maisha magumu na mabaya zaidi ya
mwanzo.
Je waweza kujiuliza ni kwanini bado yuko katika hali
aliyonayo? Je waweza kujiuliza ni
kwanini hapigi hatua kutoka pale alipo? Utakapo
muuliza aweza kuwa na majibu mengi yenye kuonyesha namna alivyokata tama, pia
aweza kukueleza majibu mengi yenye kuilalamikia familia, serikali, jamii,
marafiki na majibu mengi sana kama hayo lakini mbali na hayo ukweli ni kwamba
mtu huyo “ANAYAISHI MALENGO AMBAYO SIO YAKE” yani ni mtu anapenda kufanya kila jambo
analoliona likifanywa na watu wengine.
Katika maisha unapoweka lengo kuwa utanunua shamba ekari tano
kwaajili ya kulima nyanya au mahindi au
umeweka lengo kuwa utafungua genge ili uuze vitu mbali mbali kama vile nyanya,
vitunguu na n.k lakini baada ya muda kwasababu umemuona jirani yako amefungua
kibanda cha chipsi na wewe ukaamua kuyaishi malengo ya jirani yako hivyo
ukaamua na wewe kufungua kibanda cha chipsi kwakuwa tu unahisi kama jirani yako
anapata faida sana kwahiyo ukaamua kuachana na malengo yako ulioyaweka ya
kufungua genge au kununua ekari tano kwaajili ya kulima nyanya au mahindi.
Rafiki kuyaishi malengo ya wengine katika maisha ni utumwa
mkubwa sana unaopelekea watu wengi kubaki katika hali ya umaskini maisha yao yote, hivyo nakushauri
rafikiyangu kuwa jikubali kubali malengo uliojiwekea na chukua hatua kuyatimiza
kwani malengo yako uliojiwekea yako bora kuliko unavyofikiri, usishawishiwe na
mtu awaye yote kujaribu kubadili malengo
yako kwa kumuiga hata kama iweje chamsingi fanya kile unachokiamini kuwa
kina faida kwako na kile ambacho nisehemu ya malengo yako uliojiwekea.
Mwisho kabisa napenda nikwambie kuwa katika maisha kutokana
na bidii yako, mafanikio yako, utofauti wako, mawazo yako, “WAFANYE WENGINE
WAYAISHI MALENGO YAKO SIO WEWE KUYAIHI MALENGO YAO”
kwa makala nyingine zaidi karibu katika ukurasa wangu ulioko
facebook unaotambulika kwa jina la “ONA – MBALI” utafute kisha like na follow
ukurasa huo nawe utakuwa umejiunga na ukurasa huo.
Kwa ushauri, maoni, mapengekezo wasiliana nami kwa;
Sim: 0743782086
0679329339
EMMANUEL DAUD BLOGGER WAKO APENDAE UFANIKIWE
Post a Comment