KAMWE USIRUHUSU VIKWAZO KUHARIBU MALENGO YAKO NA RAMANI YA UNAKOELEKEA
Habari
rafiki, karibu katika ujumbe wa leo kupitia Blog hii uipendayo
ya "ONA MBALI" Blog hii yenye kukupa hamasa katika maisha yako
na kukufanya utoke katika hatua moja ya maendeleo na kwenda hatua nyingine
kubwa zaidi ya kimaendeleo.
Leo
napenda nikushirikishe habari ya vikwazo katika maisha na namna ya kufanya ili
visikuangushe bali vikufanye uwe imara kadri unavyokutana navyo katika maisha
yako.
Kuna
msemo unaosema hivi;
"kadri unavyokutana na vikwazo vingi katika maisha ndio unazidi kuwa imara
zaidi katika maisha"
Msemo
huo una maana ya kuwa unahitaji vikwazo vingi ili uzidi kuwa imara kwakuwa
pasipo vikwazo usingeliweza hata kujua fursa na kazi mbalimbali unazo zijua
sasa.
Mfano
kikwazo chepesi katika maisha ambacho naamini waweza kukielewa ni kuchapwa
fimbo unapofeli masomo darasani kama ikatokea siku ya kwanza ukachapwa kwa
sababu ya kufeli mtihani basi siku inayofuata katika mtihani utajitahidi ili
usichapwe. Kwahio vikwazo ni kama kichocheo (kwa wanachemistry huita catalyst)
cha kukufanya uzidi kuyatafuta mafanikio kwa nguvu zako zote.
Lakini
yawezekana kwako ni kinyume na maneno ninayo yasema yawezeka vikwazo kwako
vimekufanya upoteze fraha maishani mwako au yawezekana vikwazo vimekufanya
ukate tamaa ya maisha kabisa hata unajihisi huna thamani tena au yawezekana
changamoto na vikwazo unavyokutana navyo vimekufanya hata uikimbie familia yako
kwakuwa unahisi huna uwezo tena wa kuihudumia au labda vikwazo vimekufanya
uache hata kazi ambayo ilikuwa nzuri kwako au yawezekana kutokana na vikwazo
umekuwa na mawazo mengi yanayokufanya ukose raha na hata kupelekea kuumwa
maishani mwako au yawezekana vikwazo vimekufanya uwe hivyo ulivyo sasa.
Rafiki
napenda nikwambie kuwa suluhu ya vikwazo unavyokumbana navyo maishani si
kukimbia familia wala si kukata tamaa, wala si kuamua kuacha kazi, wala si
kuruhusu kuwa na mawazo kiasi hicho ulicho nacho wala si kubaki kuwa mpweke
kama ulivyo sasa bali suluhu yake ni kusimama imara na kuangalia malengo yalio
katika ramani yako ya mafanikio ambayo umejiwekea kuwa unahitaji uyafikie.
Jua
kuwa unavyo tafuta mafanikio uko katika uwanja wa vita kama komando na vikwazo
ndio maadui zako wapaswa uvishinde sio vikushinde.
Mwisho
kabisa nakuomba rafiki usiruhusu vikwazo kuvuruga malengo yako na ramani ya
unakoelekea wewe cha msingi angalia malengo yako usiangalie vikwazo
vinavyokuzunguka nawe utafanikiwa.
Napenda
nikushukuru kwa kutumia mda wako kusoma ujumbe huu katika Blog hii ya ONA MBALI
Blog bora kwaajili ya mafanikio ya maisha yako.
Usisahau
kushea ujumbe huu kwa marafiki zako ili nao wajifunze kitu kupitia ujumbe huu
wa leo.
Pia
waweza kujiunga na ukurasa wangu ulioko facebook kama hujajiunga andika
"ONA MBALI" kisha like ukurasa huo utakuwa umejiunga nawe utapata
jumbe na makala mbalimbali nitakazokuwa nikituma kila wakati.
Kwa
ushauri, maoni au shukrani waweza wasiliana nami kupitia;
Email:
daude950@gmail.com
emmarove@outlook.com
Sim:
0679329339
0743782086
Emmanuel
Daud
BLOGGER WAKO APENDAE UFANIKIWE
Post a Comment